Ujumbe wa Tanzania ukishiriki kwenye Mkutano Mkuu wa Maendeleo ya Mawasiliano Duniani, unaofanyika jijini Kigali, Rwanda; ukiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi (wa kwanza kulia), akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri Bakari (katikati) na Mkurugenzi wa Masuala ya Kisekta wa TCRA Dkt. Emmanuel Manasseh. Mkutano huo mbali na ajenda nyingine unajadili na kuweka mipango ya Maendeleo katika Sekta ya Mawasiliano Duniani ukiongozwa na Kauli mbiu isemayo “Kuunganisha Wasiounganishwa ili Kufikia Maendeleo Endelevu." Picha Na: TCRA
Wataalam wa Mawasiliano wakiiwakilisha Tanzania kwenye Mkutano Mkuu wa Maendeleo ya Mawasiliano Duniani, (ITU-WTDC-2022) unaofanyika jijini Kigali, Rwanda. Kutoka kulia ni Mwanasheria wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH) Bi. Eunice Masigati, Mhandisi Mwandamizi (WHMTH) Bi. Edith Turuka (katikati) na Meneja wa Rasilimali za Mawasiliano na Teknolojia-TCRA Mhandisi Mwesigwa Felician. Mkutano huo unaozihusisha nchi wanachama wa Shirika la Mawasiliano Duniani (ITU) unajadili mikakati ya kukuza sekta mawasiliano na TEHAMA. Picha na: TCRA.
0 Comments
Post a Comment