Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff ameagiza Daraja la Mwananchi lililopo Kata ya Mahina jijini Mwanza kuanza kukarabatiwa mara moja kufuatia kuharibiwa na Mvua zinazoendelea kunyesha jijini hapa.
Mhandisi Seff ameyasema hayo jijini Mwanza alipofanya ukaguzi wa miundombinu ya barabara iliyoharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika Mkoa wa Mwanza.


“Daraja hili la Mwananchi ni kiungo muhimu kwa wafanya biashara na wakazi wa jiji la Mwanza katika kutekeleza shughuli zao mbalimbali za kijamii na kiuchumi , hivyo nakuagiza Meneja uanze ukarabati wa daraja hili mara moja”.Aliagiza Mhandisi Seff



 

DARAJA LA MWANANCHI-MWANZA KUKARABATIWA

#Mameneja wa Mikoa wa TARURA nchi  nzima watakiwa kufanya ukaguzi wa madaraja na mifereji

Mwanza

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor  Seff  ameagiza Daraja la Mwananchi lililopo Kata ya Mahina  jijini Mwanza kuanza kukarabatiwa mara moja kufuatia kuharibiwa na Mvua  zinazoendelea kunyesha jijini hapa.

Mhandisi Seff ameyasema hayo jijini Mwanza alipofanya ukaguzi wa miundombinu ya barabara iliyoharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika Mkoa wa Mwanza.

“Daraja hili la Mwananchi ni kiungo muhimu kwa wafanya biashara na wakazi wa jiji la Mwanza  katika kutekeleza shughuli zao mbalimbali za kijamii na kiuchumi , hivyo nakuagiza Meneja uanze ukarabati wa daraja hili mara moja”.Aliagiza Mhandisi Seff

Wakati huo huo Mhandisi Seff ameelekeza Km. 4.5 za barabara ya  Igongwe-Isanzu-Kabusungu  wilaya ya Ilemela ziweke kwenye kipaumbele cha bajeti kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami.

Barabara hiyo yenye urefu wa Km. 5.8 inayoelekea hospitali mpya ya Wilaya ya Ilemela ambapo  Km. 1.3 zipo kwenye ujenzi wa kiwango cha lami.

“Ujenzi wa barabara hii utawarahisishia wananchi wa Ilemela kupata huduma za afya kwa wakati na kupunguza madhara  na vifo  vilivyokuwa vinatokana na kuchelewa kufika kupata huduma katika vituo vya afya kutokana na ubovu wa miundombinu ya barabara”.

Akiwa katika Halmashauri ya Sengerama, Mhandisi Seff alitembelea na kujionea ubovu wa barabara uliotokana na mvua katika barabara ya Tabaruka-Nyibanga-Kishinda Km.11 na Ibondo-Kasongamile-Chamabado Km. 35 na kumuelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Mwanza  Mhandisi  Makori Kisare kufanya tathimini ya uharibifu huo.

“Fanyeni tathimini ya uharibifu wa barabara hizi na muweze kurudisha mawasiliano  kwa kufanya matengenezo ya maeneo korofi na kujenga Makalavati ili barabara hizi ziweze kupitika katika misimu yote ya mwaka ”.Alisisitiza Mhandisi Seff

Vile vile, Mtendaji Mkuu huyo amewataka Mameneja wa Mikoa wote wa TARURA nchi nzima kufanya ukaguzi wa madaraja na mifereji kabla ya Majira ya mvua kuanza ili kupunguza au kuondoa kabisa madhara na uharibifu wa miundombinu ya barabara pindi mvua zitakaponyesha.