USHUHUDA MZITO WA PROF  MARK MWANDOSYA

‘’Kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja nimekuwa nikiugua na kutibiwa ugonjwa wa #COVID19 unaotokana na virusi vya CORONA(SARS-CoV-2).

Ni jinsi gani niliweza kuambukizwa ugonjwa huu kijijini kwetu Lufilyo,Busokelo,Mbeya pamoja na kuzingatia tahadhari zote dhidi ya maradhi haya Kitendawili.

Napenda Kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya uhai,zawadi ya Pasaka.Nawashukuru pia mke wangu Lucy Akiiki, watoto na wajukuu, familia ya kahigwa na Mwandosya, Madaktari,Wauguzi wangu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na Hospitali Nairobi(Nairobi Hospital) @AMREFFlyingdocs,Uongozi wa StanbicBankTz, Familia ya Balozi Chirau na mkewe Mama Rose Mwakwere wa Nairobi Kenya, Familia ya Jaji wa Mahakama ya Juu nchini Uganda Mheshimiwa Paul na mkewe Mama Grace Mugamba na ndugu na marafiki wote wanaoendelea kunitakia heri na afya njema, Asanteni sana.

Huu ni ushuhuda wangu kwamba Corona/Covid19 ipo Tanzania, tumebahatika kupita kipindi hiki cha mpito salama na kumpata Rais Mpya Mheshimiwa @SuluhuSamia,Mwenyezi Mungu amjaalie neema na Baraka tele.
Mheshimiwa #DrPhilipoMpango, Makamu wa Rais ambaye nampongeza kwa uteuzi, amepitia hayo yaliyonisibu.

Nawaomba tena kwa unyenyekevu mkubwa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu,Makamu wa Rais Mheshimiwa Philipo Mpango na Mheshimiwa Dkt Husein Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwamba tuongozwe na Sayansi na Tuungane na tushirikiane na wenzetu duniani kote katika kupambana na ugonjwa huu kama tunavyofanya katika milipuko ya magonjwa mengine kwani katika mlipuko wowote hakuna anayeweza kuwa salama mpaka wote duniani tumekuwa salama.

Maombi yangu kwa Mwenyezi Mungu ni kwamba ikiwezekana Mtanzania awaye yote aepushwe na mateso na taabu za kukabiliana na maradhi haya.

Hakika siwezi kumtakia mtu mwingine yeyote, hata aliye adui yangu mkubwa namna gani kama yupo, apate ugonjwa huu.

Tutakiane Pasaka Njema,Mwenyezi Mungu Ibariki Tanzania''.